Search This Blog

Saturday, February 5, 2011

GOMBA LA TAXI

Jana nakaa markiti namngoja mtu, nikipeleka macho naona jamaa watatu waja kila mmoja amefurisha tavu kwa taqsimu. Macho yamewakoboka wako wangu wangu kwa nakhwa. walipofika kuna taxi wakaingiya. Moja akaa mbele wawili wakakaa nyuma.

Dereva wa taxi akawaangaliya akajuwa leo mmeru yuko mjini.

"Jamaa mwaendapi?" Dereva akawauliza.

"Wewe twende tu!" Wakamjibu.

Dereva akawasha gari, akalingurumisha, kisha akalizima.

"Haya, tushafika!" Akawaambiya.

Wale wa nyuma kila mmoja akanyosha mkono wakampa pesa hao wakashuka.

Yule wa mbele akamgeukiya, akampiga kibao kimoja murwa kabisa kisha akamwambiya "We mpumbavu sana wewe!" alafu akashuka.

Nikajiambiya si haba angaa gomba halijamshika.

Akageuka akanambiya "Shoga sana yule, apeleka gari mbio ataka tuuwa!!!" huku yuwenda zake.

No comments:

Post a Comment