Search This Blog

Wednesday, February 2, 2011

Ya matatu ni mengi

Matatu zina vituko shekhe; Zenye midundo utasema waskizishwa waliyoko njiani hata si wale walio panda, kuna nyengine umekaa kwenye kiti lakini waona lami ukiangaliya chini. Si muhimu ni kufika bwana.

Juzi nikapanda matatu nikakaa upande wa kushoto, kule mwisho upande wa dirisha amekaa mwanamke chuma! amepakata mtoto, kisha kati kati yetu amekaa kijana apata kama miaka ishirini.

Matatu yenda mara kitoto kikaanza kuliya. Yule mwanamke akamlaza akamtoleya mtoto nyonyo pengine atanyamaza. Nilishtuka manake si kawaida sehemu hizi za kwetu mwanamke kutowa titi mahali popote, na hata akitowa atajifinika kwa nguo.

Mwanamke akesha kumbembeleza mtoto anyonye lakini wapi!

"Chukuwa nyonyo ama nitampa huyu mvlana ale yeye!" Ikabidi amtishie mali yake ili apate kunyonya.

Doh, nikashtuka maneno gani haya tena. Lakini ukimwangaliya mwana alivoleta zani utaelewa. Ikibidi imebidi sio?

"Nakwambiya baby nyonya ama nitampa huyu!!!" akarudiya mara ya pili.


Wapi! Nataka kumwambiya huyo mtoto pengine amechuchu, ama aumwa, hana haja kunyonya lakini nasema haina haja wacha nitazame yangu.

"Usiponyonya nitampa huyu nakwambiya!!!!" akamwambiya tena.

Wacha jamaa aje kali, "Sister kama utanipa nipe bwana sio kusema tu! Mi nishapita steji yangu kitambo nakungoja wewe uamuwe! Unkazana nitampa, nitampa! Wanipa ama hunipi nishuke?"

Ilibidi dereva aongeze mdundo, si mambo haya!

No comments:

Post a Comment