Search This Blog

Tuesday, February 1, 2011

NYUNYIZA JIJI

Siku hiyo nimefwatana na swahibu yangu maeneo ya viwanadani Nairobi; wenye jiji wakuita Indaa. Mbona siku ilikuwa inda. Jamaa amekabwa na mkojo anikazanisha mwendo ati atafuta choo utasema mgonjwa wa sukari. Namuuliza yakhe choo kitoke wapi huku? Namwangaliya komo langa'ra kwa kijassho chembamba.

Tukapiga kichochoro kimoja jamaa anvuta rasi hataki tena kwenda. Namuona pumzi matavuni
Anambiya, "Bwana hapa zitakharbatika!"
"Sasa itakuwaje" namuuliza
"Hakuna chakuwa hapa, nikukuojowa tu!"

Akalekeya ukuta na kufunguwa zipu. Hajajaza hata kikombe cha kahawa mara twasikiya

"Ai...oooh, ni nyinyi munatabiya kama ya umbwa?" Ndio hawa waitwao Kanjoo ama vipi?
"Ebu onyesha sisi choo na hapana rudisha exhibit ndani ya suruali!" Weeeeeh!.

Mimi niko? kubwaa. Namwacha jamaa yuko nyuma yuwaniandama mbio mikojo yamrukiya rukia aliya nimngojee.

No comments:

Post a Comment