Search This Blog

Thursday, February 3, 2011

MKEBE

Charo alinisumbuwa kweli ataka kazi, nikampeleka kwa jamaa yangu akapewa kazi ya kuangaliya garden.

Akaingiya makazi akapewa mzee aitwa Bakari akaambiwa ukitaka chochote wewe muone Bakari atakusaidia.

Baada ya muda Charo tumbo likamuanziya balaa, akaenda kwa Bakari kumuuliza choo kilipo. Bakari akamuonesha choo akamwambiya mfereji uko khatuwa kadhaa na chooni, atachota maji ndio aende nayo chooni.

Charo akatafuta mkebe alipopata akaenda mferejini kuchota maji akarudi na kuingiya chooni. Alipomaliza ataka kutamba, akipiga jicho mkebe hauna maji! Loh! Akatafuta tafuta namna akajisafisha huyo akarudi kazi. Alipomuona Bakari akamweleza,


"Yaonesha huo mkebe una shimo dogo maji yavuja pole pole." Bakari akamwambiya.



Siku ya pili Charo yuko kazini akashikwa tena na haja akaenda akatwaa ule mkebe wake akaenda chota maji akarudi nao choni. Mara huyo yuwaja mbio kwa Bakari acheka kweli,

Amwambiya, "Bwana Bakari, rero mkebe nkauweza! nkatamba, nkatamba kisha ndipo nkanya!"

No comments:

Post a Comment