Search This Blog

Tuesday, February 1, 2011

IMETOKA AMU


Mbona mtu akienda majuu - London, USA, Canada – akirudi huku huwa lugha imebadilika? Jamaa akizungumza maneno mawili basi la tatu ni “Yes”, “No”, ama atatiya neno la kizungu ili mradi tu.

Sasa kuna na hawa yakhe wengine wakifika Nairobi na wao wataka kuzungumza Sheng (lugha ya mtaani ya Nairobi).  Basi Famau Alhamdulillahi akafika Nairobi akawa apiga kibaruwa. Baada ya muda akapoteya haonekani kumbe amerudi zake visiwani.

Siku hiyo niko Mombasa na Jemo rafiki yangu wa kinairobi muda namshtukiya Famau huyu ndiye!

“Ah Famau abawa, assalam aleikum! “ Namwakuwa kwa furaha

Sikujuwa kumbe Jemo na Famau wajuana.

“Ah Famaa, niaje budaa! Mzee ulilostiya Costo kumbe!” Jemoo akaruka kumuamkuwa.

“Niko mazeee, nirudi mahomuuu!” Alaa? Famau azungumza sheng?

“Manze kuna day nilikuvutiya wire lakini rununu iko mteja, kwani ulichange number?” Jemo akamuuliza.

“Simu yangu nilijepewa joooo!”

Ah! Famau! Jepewa???

No comments:

Post a Comment